Wazazi katika lokesheni ndogo ya Ifwetere eneo bunge la Malava kaunti ya Kakamega wameshauriwa kuwapeleka wanao shuleni huku shule zikifunguliwa nchini kwa muhula wa kwanza 

Ni usemi wake naibu chifu wa lokesheni hiyo Paul Ochami akiwahutubia waomboleza kwenye ibaada ya maombi na mazishi ya mzee Jared Harambee Opala mapema hii leo

Ochami amewashauri wazazi pia kutumia vyema vyuo vya kiufundi vya Chombeli na kile cha Shamberere

Wakati uo huo Ochami amewasihi wakaazi wake kwa wale waliopokea jumbe tatu za kudhibitisha kadi zao za huduma number zipo tayari, kufika afisini mwake ili kuzichukua

Ni hafla iliyohudhuriwa pia na wenyekiti wawili wa mashabiki za radio wakiongozwa na mwenyekiti wa mashabiki wa kituo hiki Nelson Andanje pamoja na mwenyekiti wa mashabiki wa kituo cha radio mambo Alex Chitiavi wakiwashauri wakaazi umuhimi wa kujiunga katika makundi ya vyama hasa wakati hitaji linapotokea

By Sajida Javan

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE