Mbunge wa Lugari Ayub Savula amesema chama cha ANC kimo mbioni kuwatafuta wa vyama vingine kutoka eneo la Magharibi kunjiunga na chama hicho mbele ya uchaguzi mkuu ujao.
Akihutubia wakazi wa Butere Savula amesema siku chache zilizopita mbunge wa Malava Mosoes Malulu Injendi amejiunga na chama hicho na sasa wa pili ambaye analenga kujiunga nao ni mbunge wa Mumias Mashariki Benjamin Washiali na wengine zaidi.
Aidha amemtaka gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya kujitokeza wazi na kuweka baina mazungumzo yake na naibu wa rais dkt. William Ruto kabala ya uchaguzi mkuu.