Lubao FM | 102.2 Hz

Dhuluma za kijinsia miongoni mwa wanafunzi

Maafisa wa polisi   mjini  Kakamega   wanamsaka   mwanaume   kwa  jina  Ben Khatondi mwenye  umri wa  miaka  21 kutoka  Muraka eneo bunge la Shinyalu kaunti  ya  Kakamega  anayedaiwa  kumficha   mwanafunzi  mwenye  umri  wa  miaka   17   nyumbani   kwake  kwa  zaidi  ya   majuma  mawili  kabla  ya  kumfukuza  huku akisalia kwa njia panda mjini  Kakamega  akihofia  kurejea  nyumbani kwao Kaimosi kaunti ya Vihiga.

Kulingana  na  Carolyne  Ambalo   si jina  lake  halisi  anasema  alijipata  kwenye  mtego   wa  mwanaume  huyo   baada  ya kuukalia  mtihani  wake  wa  darasa  la  nane mwaka  wa  2019 katika  shule  ya  msingi  ya  Buhunyilu  na  baada  ya  karo  ya  kujiunga  na  shule  ya  upili   kushindikana  ndipo  alisafiri  hadi  Muraka   kwa  mjomba  wake  ambako  amekuwa  akiishi; kabla ya kukutana na Ben  Khatondi  ambaye  ni  mshukiwa  na kumlaghai  awe  mpenziwe  kuwa  angelimsaidia  kurejea  shuleni.

Baada  ya  kuishi  naye kwake  kwa  majuma  mawili  mapema  leo akamtoa  nyumbani  huku akimweleza  alikuwa  anasafiri Kisumu na  hivyo  basi   angelimuhitaji baada  ya  kurejea.

Ni kisa ambacho kimekashifiwa vikali na wakaazi wa mji wa Kakamega wakiongozwa  na  Maleb  Khatioli huku  wakiwataka   wazazi  kuajibikia  wanao haswa  msimu  huu  wa  janga  la  covid  19 ambapo  nyingi  ya  familia  zimetelekeza  wanao na  kuwataka  maafisa  wa  polisi kuharakisha na kumtia  mbaroni  mshukiwa huku wazazi  wa  msichana  huyo   john  milimu  na  jackiline  milimu wakihitajika  kufika  kituo  cha  polisi  cha  Kakamega  ya  kati  kumchukuwa  mwanao.

Kaunti  ya  Kakamega  kwa  kipindi  cha  miezi sita  imerekodi  idadi  ya  juu  ya  visa  vya   kudhulumia  kwa  watoto  ikipata  hadi  asilimia  37  huku  wingi  wa  visa  hivyo  vikitekelezwa  na  watu  wa  karibu  sana  wa  wasiriwa

By Lindah Adhiambo

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE