Gavava wa kaunti ya Kakamega Wycliffe Ambesa Oparanya pamoja na Naibu Gavana Phillip Kutuma na Mwakilishi wadi wa Sango Kennedy Kilwake  hii leo wamezuru eneobunge la Likuyani kwa minajili ya uziduzi wa baadhi ya miundo misingi eneo hilo

Hafla hiyo ambayo imefanyika katika ofisi za kaunti wadi ya Sango Oparanya amezindua barabara ya kutoka Sango kuelekea Kongoni  ambayo inawekwa Lami ili kuimarisha usafiri eneo hilo

Kando na hayo Oparanya amegusia  swala la ukulima ambapo wakaazi wa Likuyani wanatarajia kupata mbolea kwa bei nafuu ili kuimarisha sekta ya kilimo

Kuhusu swala la mgomo wa madaktari gavana Oparanya amesema kuwa Mikakati kabambe imewekwa kuhakikisha kwamba wanamaliza mgomo huo.

Story by Samson Nyongesa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE