Kuna haja ya mifumo inayo simamia uchaguzi nchini kufanya mipangiliyo yao mapema kabla ya uchaguzi ili waweze kuwa na malengo yaliyo bora kwa jamii ya wakenya. Huu ni usemi wake askofu wa jimbo katoliki la Kakamega askofu Joseph Obanyi Sagwe akuwahutubia wanachama wa shirika la Haki na Amani na washikadau kutoa mashirika mbalimbali nchini

Askofu Obanyi anawaelezea washikadau wa tume huru na uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC kuwa wazi wakati wanapo fanya kazi yao kabla na baada ya uchaguzi amewaelezea kuwa ni hao tu watakao waweka wazi wakenya kuhusiana na uchaguzi mkuu na kuleta Amani.

Hata hivyo Askofu Obanyi Amesikitikia changamoto ambazo tume hiyo inapitia na kuwashauri wafanyikazi wa tume huru na uchaguzi na mipaka nchini kufanya kazi bila kuangazia changamoto wanazopitia ili kuangalia wananchi wanao wahudumia

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE