Mbunge wa kwanza kwenye kaunti ya Transnzoia Ferdinard Wanyonyi amependekeza idara ya afya kurejeshwa kwa serikali kufuatia hatua ya serikali za magatuzi kufeli kuwajibikia sekta hiyo ipasavyo.

Akizungumza na wanahabari mapema leo katika eneo bunge lake,Wanyonyi amesema serikali za kaunti zimefeli kuwajibikia sekta ya afya ipasavyo,akisema kuwa ipo haja ya idara ya afya kurejeshwa katika serikali ya kitaifa ili kuimarishwa zaidi.

Wanyonyi aidha amesema kuwa kuchelewa kukamilika kwa ukarabati wa barabara ya Namanjalala-kwanza kumechangiwa na upungufu wa fedha kutoka kwa serikali hali ambayo imelemaza miradi mbali mbali nchini.

By Sharon Lukorito

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE