Wafanyibiashara sokoni Makunga eneobunge la Mumias Mashariki wanalalamikia ukosefu wa maji sokoni humo

Wafanyibiashara hao sasa wanahofia mkurupuko wa Magonjwa kutokana na tatizo hilo

Vilevile amesikitikia mazingira duni wanamoendeshea biashara zao huku taka zikijaa kote sokoni

Wafanyibiashara hao aidha hutatizika haswa masaa ya jioni baada ya taa ilowekwa pale na serikali ya kaunti ya Kakamega kufeli kufanya kazi siku kadhaa zilizopita

Sasa wanaitaka serikali ya kaunti ya kakamega kuingilia kati na kutatua tatizo hilo ikitiliwa mkazo ushuru wa juu wanaotozwa

Haya yanajiri siku chache tu baada ya nyuki amabao wamehamia sokoni humo kuwafurusha sokoni humo huku wakimvamia na kumjeruhi vibaya  mojawapo wa wafanyibiashara wa soko hilo

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE