Baadhi ya vyongozi pamoja na wakaazi wa mtaa wa Makunga wilayani Mumias Mashariki sasa wanataka usimamizi wa hospitali ya Makunga kubadilishwa kama njia pekee ya kuboreshewa kwa huduma katika kituo hicho Cha afya

Wakiongozwa na Caleb Okumu mwenyekiti wa wanabodaboda Makunga Corner Stage vyongozi hao wanausuta uongozi wa hospitali hiyo kwa utepeteveu

Wale wasimamizi wa hospitali wabadilishwe kwa sababu wagojwa kwa mara mingi wanasaidiwa tu na watchman hasa sana mama wajawazito

Wakaazi hao aidha wametaja baadhi ya vifo vya wagonjwa kikiwemo Cha hivi punde Cha mhasiriwa wa ajali wiki iliyopita wakivihusisha na  uzembe kwenye usimamizi wa hospitali hiyo 

Wagojwa hawaudumiwi na wanakufa bila ata kushughulikiwa. hata kama akuna matibabu ya kutosha ni vizuri hospitali kuelekeza mgojwa katika hospitali nyingine

.Wakaazi hao wamedokeza kuwa wagonjwa pamoja na wafanyikazi wa hospitali hiyo hukumbana na masahibu ya yakiwemo kunyimwa chakula huku usimamizi ukisalia kimya kuhusu swala hilo

Juhudi zetu za kuzungumza na wakuu wa hospitali hiyo ya Makunga hazikufua dafu baada ya afisa anayesimamia kituo hicho kudinda kuzungumzia swala hilo 

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE