Pendekezo  la  kurejesha  adhabu  ya  kiboko  shuleni  linaonekana  kuwavutia  baadhi  ya  wazazi  huku  wakisema  kwamba  itasaidia  kumaliza  visa  vya  utovu  wa  nidhamu  kwa  mwanafunzi.

Kwa  upande  wake  bwana  Isaac  Taly  mkaazi  wa  Buyangu  katika  wadi  ya Isukha  Kaskazini  kaunti  ya  Kakamega,  anasema  kwamba  lawama  kubwa  inamwelekea  mzazi  kwa  kumdekeza  mwanaye  na  kumpandika  jina  huku  akijiona  ametosha.

Hata  hivyo  naye  bwana  Patrick  Mutsami  anafichua  kwamba  mzazi  hakuchukua  jukumu  lake  alipokuwa  na  mwanaye  nyumbani  wakati  wa  likizo  refu  ya  kipindi  cha  covid-19  na  kuunga  mkono  kurejeza  adhabu  ya  kiboko  shuleni


Story by Sajida Wycliffe

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE