Chama cha kutetea masilahi ya walimu nchini KNUT kaunti ya Kakamega chafanya uchanguzi huku aliyekuwa mwenyekiti na katibu mkuu Patrick Chungani na Argadious Liyayi kwa mtawalia wakichaguliwa tena
Wakizungumza baada ya kuchaguliwa afisi hiyo ya kaunti ikiongozwa na mwenyekiti wake Patrick Chungani imeahidi kuendelea kutetea masilahi ya walimu bila kuogopa vitisho kutoka kwa serikali na tume ya kuajiri walimu TSC
Ni usemi ulioungwa mkono na katibu mkuu Argadious Liyayi na mwakilishi wa chama hicho katika kanda ya magharibi Emily Neuto waliokariri kuwa ni umoja wao tu utawezesha walimu kupata haki yao na kufanya kazi kwa mazingira bora
Mwakilishi wa wamama aliyechaguliwa ni Janet Wasike , Tungani Ashikhule akiridhika na wadhifa wa naibu mwenyekiti miongoni mwa nyidhifa zingine
BY Boaz Shitemi