Idadi ya virusi vya korona  inaendelea kuongezeka sawia na wale wanaoendelea kupona. Hii leo Visa vya walio ambukizwa virusi vya corona vimekuwa 183 na kufikisha jumla ya watu walio ambukizwa  8,250 chini ya saa ishirini na nne ambapo sampli 2,061zilifanyiwa vipimo 

Waziri wa afya Dkt. Mutahi Kagwe hii leo alieleza kuwa kutoka kwa visa hivyo 183 ni kuwa 177 ni wa kenya na 6 wakiwa raia wa kigeni. Wanaume walio ambukizwa ni 119 na wanawake wakiwa 64 na huku walioambukizwa wakiwa kati ya miaka 4 na miaka 75.

Nairobi inaongoza  kwa visa 100  ,machakos ikiwa na visa 37 ,kiambu  visa 14 ,Mombasa visa 13  ,Kajiado visa 11 ,Nakuru visa 5 na Busia ina visa 3.

Wagonjwa 90 wameruhusiwa kwenda nyumbani  na kufikisha idadi ya walio pona 2504 huku watu watatu wakiaga dunia na kufikisha  idadi ya 167 waliofariki kutokana na ugonjwa huo . Waziri Kagwe amewaonya wakenya dhidi ya kuwa watepetevu  hasa baada ya rais Uhuru Kenyatta kufungua usafiri  kutoka  kaunti moja hadi nyingine

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE