Kufwatia ongezeko la visa vya dhulma dhidi ya watoto katika jamii haswa siku za hivi punde mshirikishi wa usalama Kanda ya magharibi Esther Maina amewaonya wazazi watakaopatikana wakihusika kwenye visa hivyo kuwa watakabiliwa kisheria

Kwenye kikao na wanahabari afisini mwake Maina amesema kuwa kama vitengo vya usalama wanafanya wawezalo kukomesha visa hivyo 

Hata hivyo amewataka waathiriwa kuripoti pindi wanapotendewa unyama huo ili hatua za dharura zichukuliwe

machifu dhidi ya kusuluhisha kesi za ubakaji nje ya mahakama  akisema kuwa hii inazuiya waathiriwa kupata haki

Amewataka wazazi kumakinika na usalama wa watoto wao haswa wakati huu ambapo wako nyumbani kwa likizo fupi

Haya yanajiri huku shirika lisilo la kiserikali linaloangazia dhulma dhidi ya watoto la Survivors of Child Sexual Abuse likionyesha kuwa watoto 2 kati ya 4 hunajisiwa kila siku haswa kaunti ya Kakamega huku visa zaidi ya 200 vikiripotiwa kwa muda wa miezi 3 iliyopita

Shirika Hilo aidha limedokeza kuwa wingi wa visa hukosa kuripotiwa kwani hushugulikiwa katika kiwango cha kijamii

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE