Wafanyibiashara katika soko la Ingolomosio  eneo bunge la Shinyalu kaunti ya Kakamega  wamelalamikia ukosefu wa vyoo na maji kwenye soko hilo na kuitaka serikali ya kaunti ya Kakamega kuwajengea vyoo na maji kuzuia mkurupuko wa magonjwa yanayotokana na uchafu.

Wakiongozwa na Dinah Chenyeka wafanyibiashara hao wanasema kuwa wanapitia changamoto nyingi wanapotaka kwenda haja kwani inawabidi kwenda vichakani kujisaidia

Wakati huo uo wanasema kuwa soko hilo halina Maji ya kutumia hasa wakati huu wa corona huku wakihofia kupatwa na ugonjwa unaotokana na uchafu huku wakiitaka serikali ya kaunti ya Kakamega kuingilia kati kwani wanalipa ushuru kama wakenya wengine.

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE