Wakaazi eneobunge la Mumias Mashariki wametakiwa kujitokeza na kupata chanjo dhidi ya virusi vya Corona ili kujikinga  kutokana na ugonjwa huo 

Afisa mkuu wa afya eneo hilo la Mumias Mashariki William Malakwen amekanusha uvumi kuwa huwenda chanjo hiyo ina madhara akiitaja kuwa salama

Afisa huyo wa afya amesema kuwa wanaolengwa ni watu wazima pekee akionyesha kuridhika na namna zoezi hilo linavyoendelea eneo hilo

Kuhusu chanjo dhidi ya ugonjwa wa ukambi iliyokamilika siku chache zilizopita Malakwen amehoji kuwa zaidi ya asilimia 90 ya watoto kutoka kaunti hiyo ndogo wamepata chanjo hiyo 

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE