Wakazi wa wadi ya Marama Magharibi eneo bunge la Butere kaunti ya Kakamega wameitaka serikali ya kaunti kukamilisha miradi iliyoahidiwa na gavana Wycliffe Oparanya kabla ya kipindi chake cha kuhudumu kukamilika

 Wakiongea kijiji cha Lwaminyi wakati wa kutoa maoni kuhusu maendeleo ya kaunti, wakazi hao wanasema maswala ya barabara na maji hayajashughulikiwa ipasavyo

Hata hivyo mwakilishi wa wadi hiyo Boaz Omukunde Saitama ambaye alihudhuria kikao hicho amewataka wakazi kuwa na subira akisuta uchelewashaji wa fedha za serikali

Saitama amewataka wakazi kuona kwamba wanaunga mkono BBI akisema ndio suluhu kwa changamoto za miradi mashinani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE