Kati ya shule 144 zilizokalia mtihani wa kitaifa KCPE eneobunge la Malava
kaunti ya Kakamega shule ya msingi ya mtakatifu  Teresa Isanjiro ndio
imeongoza na alama  349 katika shule za serikali huku St Imaculate primary
ikiongoza katika shule za kibinafsi na kuzoa alama 351

Haya ni kwa mujibu wa mkurugenzi wa elimu kaunti ndogo ya Malava Isaac
Kiprais ambaye amohoji kuwa elimu katika eneo hilo  imenawiri kutokana na
msaada aliopokea kutoka kwa mbunge wa Malava Mosses Malulu wa vitabu vya
kutosha pamoja na madarasa yaliojengwa katika shule mbalimbali za eneo hilo

Aidha Kiprais amehoji kuwa katika mtihani wa kitaifa wa kitato cha nne KCSE
uliokamilika wasichana wengi waliokuwa na uja uzito walijifungua wakati wa
mtihani huo hasa siku ya jumamosi.


Hata hivo Kiprais amekariri kuwa ugonjwa wa korona umeadhiri pakubwa masomo
ya baadhi ya wanafunzi ambao wamepata alama 200 kurudi chini


By Richard Milimu

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE