Familia moja kutoka kijiji cha Bugina Kaunti ya Vihiga, inaomboleza kifo Cha mmoja wao, Elfas Nengo Indangasi, baada ya kukatwa na kundi la vijana linaloaminika kuwasumbua wanakijiji hao.
Kulingana na Caith Desire, mmoja wa familia hiyo, Nengo alisikia sauti ya watu wakitembea nje mwendo wa saa mbili usiku kisha kutoka nje kutaka kujua ni nini kilikuwa kinaendelea kabla ya kukatwa katwa kisha kuaga alipokuwa anakimbizwa hospitalini.
Kwa sasa mwili wa marehemu umelazwa katika chumba cha wafu cha hospitali ya Kaimosi Jumuia huku uchunguzi ukianzishwa.
Story by Alovi Joseph