Viongozi wa kidini katika kaunti ya Kakamega chini ya mwavuli wa Kakamega Mashinani Pastors Fellowship wameikashifu serikali kwa malumbano ya kisiasa ambayo yamepelekea kufungwa kwa makanisa kwa kusingizia Corona
Mwenyekiti askofu Zablon Mukoshi amesema inashangaza sehemu zingine kusalia wazi huku makanisa yakifungwa
Askofu Mukoshi amesema kuna siasa katika swala hili hasa kumzuia naibu wa rais William Ruto kutembelea makanisa
Wanasema haiwezekani kufunga makanisa huku sehemu za burudani na shule hasa za kutwa zikiendelea
By Lindah Adhiambo