Onyo kali imetolewa kwa wauzaji wa pombe aina ya chang’aa na vijana wanaojihusisha na mchezo wa kamari uliopigwa marufuku nchini
Ni kauli yake chifu wa lokesheni ya Kambiri Caleb nNatili akizungumza na kituo hiki baada ya mkutano wa baraza la kiusalama kwandaliwa leo katika kijiji cha Bukhaywa,wadi ya Isukha kazkazini,eneo bunge la Shinyalu kaunti ya Kakamega
Natili amewaonya wenyeji wa Bukhaywa dhidi ya kujiusisha na unywaji wa pombe haramu na kujihusisha na mchezo wa kamari karibu na maeneo ya shule swala ambalo huenda likachangia kudorora kwa usalama eneo hilo na kuchangia matokeo duni kwenye shule zilizo karibu na mahala shughuli hizo haramu huendelea
By Javan Sajida