Kuna hofu ya mkurupuko wa magonjwa kwenye soko la Makunga wilayani
Navakholo iwapo hatua za dharura hazitachukuliwa

Kulingana na wafanyibiashara sokoni humo hii ni kutokana na mrundiko wa
taka ambazo zimekaa kwa muda wa miaka 2 sasa

Licha ya soko hilo kugeuka makaazi ya wanyama hatari na hata nyuki
wafanyibiashara hao walohamia maeneo ya  nje ya soko sasa wanadai uvundo
mkali kuwafuruaha toka sokoni humo

Kando na hayo wafanyibiashara hao wanalalamikia utovu wa usalama sokoni
humo wakiwanyoshea kidole Cha lawama polisi kwenye kituo cha Makunga kwa
kutowapa usalama wa kutosha

Soko Hilo la Makunga limesalia bila kujengwa kwa zaidi ya miaka 30 sasa
licha ya ujio wa ugatuzi huku tetesi zikisema kwamba Ni kutokana na
mzozo wa umiliki wa soko hilo  baina ya manispaa ya kaunti ndongo ya
Navakholo na Ile ya Mumias Mashariki

Story by James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE