Ni sharti tume ya kuajiri waalimu inchni  kuharakisha kuwapandisha vyeo waalimu walio hitimu kufanyiwa hivyo.

Akizungumza katika eneo bunge la Bumula kaunti ya Bungoma, mwenyekiti wa chama cha kutetea masilahi ya  walimu wa shule za msingi Bungoma Mashariki Agrey Namis,i amesema kuwa tume ya kuajiri waalimu huchukua muda mrefu kupandisha walimu walio hitimu katika viwango tofauti kulingana na masomo waliyo nayo.

Namisi pia ametaka mgurugenzi mkuu wa tume ya kuajiri waalimu nchini Nancy Macharia kudhibitisha sitakabadhi za walimu hao wanao sitahili kupandishwa vyeo, na amesema sharti hilo litekelezwe chini ya miezi sita’  ‘ 

Aidha Namisi amelipinga moja kwa moja  swala la waalimu kutakiwa kuwa na diploma pekee bali si kuwa na shahada kutoka katika chuo kikuu huku akisema  kuwa itaathiri waalimu wa shule zaupili pakubwa.

By Hillary Karungani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE