Hofu imetanda katika mtaa wa Eshiakhulo eneobunge la Mumias Mashariki baada ya mwili wa mwanamme mmoja kupatikana ukiwa na kamba shingoni Kwenye uwanja wa shule ya upili ya Eshiakhulo

Mwili huo ulopatikana Leo asubuhi ulikuwa na kamba shingoni dhibitisho kuwa mwendazake alijinyonga

Chifu wa kata ndogo ya Khaimba Mary Njaya amesema kuwa mwili huo ulikuwa na majeraha shingoni

Chifu huyo amehusisha kifo hicho na mizozo ya kifamilia akiwataka wakaazi kutafuta mbinu mwafaka ya kusuluhisha migogoro hiyo 

Mwili wa mwendazake umeenda kuhifadhiwa kwenye makafani ya hospitali ya kimishenari ya St Mary’s Mumias

Story by James Nadwa

sadmin

By sadmin

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE