Hali ya simanzi imetanda katika kijiji cha muraka kata ya ilesi eneo bunge la shinyalu baada ya mwili wa aliyekuwa mkuu wa nyumba kumi katika kata hio kupatikana ameaga kwa njia tatanishi

Kulingana na majirani walioshuhudia, mwili wa richard khayumbi ulipatikana mapema hii leo kitandani mwake huku mwili wake ukiwa umechanika na kutoa harufu mbaya. Inakisiwa kuwa khayumbi alionekana siku ya jumapili kwa mara ya mwisho

Hali hio ya taharuki imewashangaza wakaazi huku wakiomba serikali kuingilia kati kwani wanahofia usalama wao ikiwa mkuu wa nyumba kumi anaweza kuangamia kwa njia kama hio

Akidhibitisha kisa hicho, mkuu wa nyumba kumi kaunti ndogo ya shinyalu hussein muhanji amesikitikia kisa hicho huku akikisi kuwa khayumbi aliuawa na watu wasiojulikana kufuatia msako walioufanya juzi wa majambazi katika kata hio

Hata hivyo, muhanji alisisitiza kuwa hao kama nyumba kumi hawatarudi nyuma katika kuwaekea usalama wakaazi wa eneo hilo

Story by Tomcliff Makanga

sadmin

By sadmin

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE