Vyongozi mbalimbali wanazidi kutoa hisia zao kuhusu masharti mapya alotangaza rais kama njia mojawapo ya kukabili msambao wa virusi vya Corona

Afisa msimamizi wa maswala ya jinsia na watoto kaunti ya Kakamega Peninah Mukabane amewataka wanasiasa kutoingiza siasa kwenye swala hilo

Mukabane amekanusha masharti hayo kuulenga mrengo wowote wa kisiasa na kuwataka Wakenya wote kuyakumbatia 

Afisa hiyo hata hivyo amewatahadharisha polisi dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi jinsi ilivoshohudiwa hapo awali

Hata hivyo Mukabane amewataka walimu kutowabagua watahiniwa haswa watakaopatikana na ujauzito wakati huu wanapojiandaa kwa mtihani wao wa kitaifa

Haya yanajiri huku zaidi ya watahiniwa milioni4 wakitarajiwa kuukalia mtiani wa kitaifa kote  nchini baadaye wiki hii

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE