Mwanaume mwenye umri wa miaka 45 kwa majina Andrew Soita Webo kutoka kijiji cha Luichi kata ya Chegulo eneo bunge la Malava kaunti ya Kakamega  ameteketezwa na  wananchi wenye hamaki na kufariki baada ya kupatikana akiwa amemjinja ng’ombe ambaye alikuwa ameibwa kutoka boma moja sehemu hiyo.

Wakizungumza na kituo  hiki wakaazi wa eneo hilo wakiongozwa na mzee wa mtaa Charles Webo wamehoji kuwa mwanaume huyo alimchinja ng’ombe huyo ndani ya nyumba yake jambo ambalo limewaacha vinywa wazi kabla ya kumtekeketeza.

Akithibitisha kisa hiki chifu wa eneo hilo Juma Inzai amehoji kuwa mabaki ya mwili wa mwenda zake yamepelekwa kwatika chumba la kuifadhi wafu cha hosipitali ya Webuye.

Hata hivyo Inzai amelaani kitendo hicho na kuwaonya wananchi dhidi ya kujichukulia sheria mkononi mwao.

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE