Gavana wa kaunti ya Kakamega Wycliffe Oparanya ameitaka wizara  inayosimamia wafanyikazi kupitia  kwa bodi ya kuajiri wafanyikazi katika kaunti hiyo kuweka mfumo  mwafaka utakaosaidia kubaini  iwapo watu wanaopewa nafasi hizo wamehitimu au la

Akizungumza afisini  mwake katika  kikao na walimu wa vyuo vya kiufundi na ECDE kutoka kaunti  hii ya Kakamega, Oparanya anasema ipo haja kwa  bodi inayowapiga msasa na kukusanya maombi ya kazi kuwa makini wakati wanapokea maombi hayo ili  kuepukana na kuajiri wafanyikazi wasiohitimu kutokana na stakabadhi gushi wanasokabidhiwa bila kumakinika.

Gavana huyo aidha ameitaka bodi hiyo kuiga mataifa na  kaunti zingine kwa kuweka  mfumo ama teknojia maalumu itakayosaidia kubaini iwapo  stakabadhi zinazowasilishwa na wanaotuma maombi ya kazi  zimefanyiwa ukarabati au la akisema kwa kufanya hivyo kutasaidia kupunguza idadi ya wanaopata kazi kwa njia isiyokuwa halali na hivyo kusababisha kupotea kwa mamilioni ya pesa kwa kuwalipa watu wasiohitimu..

Oparanya amesikitikia idadi kubwa ya wafanyikazi wa kaunti hiyo ambao wamekuwa wakipokea mishahara ya bure  na hata kuwa vigumu  kuwatoa katika orodha wakati wanapogundulikav akidokeza serikali yake haitalaza damu kamwe hadi mbinu mahususi ifuatwe katika kuajiri wafanyikazi wa kaunti hii.

By Lindah Adhiambo

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE