Gavana   wa  kaunti  ya  Kakamega  Wycliffee  Oparanya   amesikitikia  idadi  ndogo  ya  wanafunzi  ambao  hujiunga  na  vyuo   vya  ufundi  katika  kaunti  hiyo   licha ya serikali yake kuweka mikakati kupitia kwa wizara ya elimu kwa kutenga  shilingi  10,000 kwa  kila mwanafunzi  kila  mwaka ambaye hujiunga na vyuo hivyo  huku  akiwataka  wazazi kutoka kaunti hiyo kukumbatia  elimu ya vyuo hivyo kama njia moja ya kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa kujitegemea maishani.

Akihutubu katika uga wa Bukhungu mjini Kakamega kwenye hafla  ya  kuzikabidhi  shule  za  chekechea vifaa vya kuwasaidia masomoni vikiwemo  viti  na  meza  gavana  Oparanya  amesema  idadi  ya  wanafunzi wanaojiunga  na  vyuo  vya  kiufundi  kaunti  hii ni  ya  chini  mno tangu mfumo wa ugatuzi uanzishwe ukilinganisha  na   wale wa shule za chekechea

Kuhusu swala la miundo misingi gavana Oparanya   amesema   serikali  ya kaunti ya Kakamega   imejitahidi kuhakikisha ipo ya kutosha ili kupiga  jeki   masomo  shule za chekechea  na  vyuo  vya  kiufundi   mbali na kuwaajiri  walimu  zaidi na kuongeza mishahara yao

Ni shilingi  milioni 54.5 ambazo  zimetumika  kutengeneza  viti  hivyo  vitakavyo  wafaidi  wanafunzi   124,000 kutoka  shule mia 266  wa shule za chekechea  zilizoko  maeneo bunge   kumi  na  mawili  ya  kaunti  hii, shilingi  milioni  74  zikitengwa  kununua  vitabu  vya  kusoma  katika  shule  za  hizo na  vyuo  vya  ufundi,  akipongeza  vyuo  vya  ufundi kwa  kuutumia  ujuzi  wao  kuunda  vifaa hivyo

By Lindah Adhiambo

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE