Muungano wa kitaifa wa wauguzi nchini wa ‘Kenya Progressive Nurses Association’ umeitaka serikali kuu na zile za kaunti kutumia fedha ambazo hupata kwa wahisani wa nje kwa kuegeza pakubwa kwenye vyumba vya kuwalaza wagonjwa mahututi haswa kwenye mitambo ya kuhifadhi na kutoa hewa safi (oxygen) ili kukabili uhaba uliyopo wa hewa hiyo nchini
Akizungumza mjini Kakamega, mwenyekiti wa muungano huo nchini Michael Nyongesa, amesema kutokuwepo kwa mpangilio maalum kwenye matumiza ya fedha za humu nchini umechangia nyingi ya hospitali za humu nchini kukosa kukabiliana na dharura ya janga la korona
Haya yajiri baada ya waziri wa afya kaunti ya Kakamega Collins Matemba kusema kuwa kaunti hiyo imejianda vilivyo kuona kuwa kuna hewa ya oksijeni kwa hospitali za eneo hilo
Hata hivyo Nyongesa amedokeza kuwa muungano huo uko tayari kushirikiana na serikali za kaunti kuhusiana na swala hilo iwapo watapewa nafasi
By Richard Milimu