Kasisi mkuu kanisa la Baptist mjini Bungoma Clapperton Mchanga amewarai viongozi nchini kuwa na mshikamano tunapoelekea uchaguzi mkuu mwakani.

Akizungumza kwenye hafla ya maombi  kanisani mwake mjini Bungoma  kasisi huyo amesikitikia vuta ni kuvute za kisiasa za viongozi wa haiba ya juu nchini zinazoendelea kushuhudiwa huku akitilia hofu kuwa huenda  zikaleta migogoro ya kisiasa  nchini.

Kasisi Clapperton amehoji kuwa ni wajibu wa kila kiongozi kuheshimu ajenda  za mwenzake huku akisema kuwa siasa za viama zilibuniwa kuleta uiyano na demokrasia wala sio kugawanya  wana nchi kama inavyoshuhudiwa kwa sasa.

Mtumishi huyo wa Mungu aidha ameitumia fursa hiyo  kuwatahadharisha viongozi wenzake wa kidini na vijana dhidi ya kujihusisha na siasa za kimirengo na matusi kama mojawapo wa njia za kupunguza joto la kisiasa nchini.

Ikumbukwe kuwa siku  za  hivi karibuni viongozi wakuu serikalini akiwemo naibu wa rais DKT William Samoei Ruto na waziri wa usalama wa ndani daktari Fred Matiangi wameonekana kutofautiana hadharani kutokana na swala la haswaa ni nani anafaa kuwekea ulinzi naibu wa rais William  Ruto  swala ambalo limeonekana kuuzambaratisha hata zaidi uhusiano kati ya rais Kenyatta na naibu wake.

By Hilary Karungani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE