By Charles Etale
Uchaguzi mkuu wa mwaka ujao unapokaribia, Josphat Wakukha mwakikishi wadi wa kabras kusini, amesisitiza dharmira yake kuu kwa wenyeji wa wadi hiyo. Wakukha ameyasema hayo alipokuwa katika hafla ya michezo ya kudumisha amani kwenye Shule ya msingi ya Chevoso, eneo bunge la Malava.

Ikiwa ni takriban mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027, viongozi kutoka maeneo mbalimbali wamezidi kushabikia maendeleo wanayoyatekeleza. Mwakikishi wadi wa kabras kusini Josphat wakukha ameweka wazi azma yake ya kuzidi kuwasaidia wananchi wa eneo hilo
Chumba cha kina mama wajawazito cha Shikhome,ambacho ni cha Kwanza katika wadi ya kabras kusini kinaelekea kutamatishwa ili kuhudumia wananchi anavyoelezea mwakikishi Josphat wakukha.