Viongozi mbalimbali kutoka eneobunge la Mumias Mashariki wanazidi kulalamikia utovu wa usalama ambao umekithiri eneo hilo 

Mwanasiasa Paul Makokha amekuwa wa hivi punde kushtumu hali hii akilaumu idara ya usalama eneo hilo kwa utepetevu

Makokha amesema kuwa huwenda polisi wanashirikiana na wahalifu kuwahangaisha raia akishangaa mbona wezi hao hawakabiliwi kisheria

Kiongozi huyo amesikitikia kiwango cha juu cha fedha zinazotengewa idara hiyo ilihali wakaazi wanazidi kuishi kwa hofu akiongeza kuwa hili pia ni tishio kwa wawekezaji

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE