Wazazi wametakiwa kuwajibikia malezi ya watoto kukabili changamoto ya visa vya uhalifu vinavyoendelezwa na vijana wa umri mdogo
Akiongea kwenye hafla ya kuwekea wakfu mtoto wa askofu Odongo Swati katika eneo la Tumaini kata ndogo ya Ematiha eneo la Navakholo, askofu Makeyi Otisa wa New Call Pentecostal Church amesema wengi wa wazazi wamechangia utovu wa nidhamu kwa kutowaelekeza watoto kanisani
Familia ya askofu Odongo ilikuwa na shukrani kwa mwenyezi Mungu kwa zawadi ya mtoto huku wakihimiza wazazi wa kisasa kuendeleza uzao bila kujiweka kwa kupanga uzazi
By Linda Adhiambo