Conceptual shooting of shoes. Old shabby shoes in comparison with new and expensive ones.

Mwanaharakati wa maendeleo eneobunge la Bumula kaunti ya Bungoma Jack Wanami ametoa wito kwa walio na uwezo katika jamii kuwafaa wasiojiweza  na kuwainua kimaisha

Akizungumza katika eneobunge lake Wanami amesema kuwa akishirikiana na washikadahu mbalimbali  watahakikisha kuwa wakaazi wote wasiojiweza wanapokea huduma za afya kupitia hazina ya matibabu nchini NHIF

Amehoji kuwa wanao mpango vilevile wa kuwapa elimu watoto kutoka familia zisizo jiweza akiwashukuru washirika wakiwemo vyongozi wa kisiasa wanaokumbatia mpango huo

Mwanaharakati huyo anayekimezea kiti cha eneobunge la Bumula amepuuzilia mbali madai kuwa polisi wanatekeleza majukumu yao kimapendeleo haswa kwenye vita dhidi ya ugonjwa wa covid 19 akiwataka wapinzani wake kuzingatia ajenda kwa wakaazi wala sio uvumi

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE