Huku shughuli za masomo zikiingia juma la pili katika taasisi zote za elimu nchini zaidi ya vijana 40 wamepata fursa ya kujiunga na chuo cha kiufundi cha Shamberere kupitia kwa afisi ya mwakilishi wa wadi ya Butali Chegulo katika eneo bunge la Malava.
Akizungumza baada ya kukamilika kwa zoezi la kuwasajili wanafunzi hao mwakilishi wa wadi hiyo Kevin Mahelo amehoji kuwa kwenye awamu hii ya pili wameweza kuwasajili zaidi ya wanafunzi 40 huku akiwapongeza wazazi eneo hilo kwa kuitikia mwito huo na kuweza kuwaleta wanao kujiunga na taasisi hiyo.
Kwa upande wao wazazi wakiongozwa na David Shimaka wameonyesha furaha yao kutokana na mpango huo huku wakimshukuru mwakilishi wadi huyo kwa kazi nzuri anayofanya hasa katika sekta ya elimu.
Hata hivyo Mahelo ametumia fursa hiyo kumkosoa rais Uhuru Kenyatta kufuatia matamshi aliyoyatoa hivi maajuzi kwenye hafla ya mzishi kule Mululu kaunti ya Vihiga akisema kuwa ni njia mojawapo ya kueneza siasa za ukabila.