Serikali ya kaunti ya Kakamega inafanya kila iwezalo kuzisaidia kamati simamizi za  masoko sehemu mbalimbali katika kaunti hiyo kama njia mojawapo ya kuimarisha masoko hayo

Kwenye mahojiano ya kipekee na idhaa hii mshauri serikali ya kaunti ya Kakamega kuhusu uongozi Ali Musa Chibole hata hivyo ametaja kucheleweshwa kwa pesa kutoka  serikali kuu kumeathiri usimamizi huo 

Chibole amesema kuwa kama serikali wanajaribu kutatua tatizo hilo

Chibole aidha amekiri kuwepo kwa changamoto  katika kurekebisha miundomsingi haswa daraja zinazosombwa na maji ila ameahidi swala hilo kuangaziwa hivi punde.

Haya yanajiri huku daraja kadhaa eneobunge la Mumias Mashariki zinazounganisha kaunti hiyo ndogo na Ile ya Lurambi pamoja na ya Butere kwenye mitaa ya Maraba-Matende na Isango -Esokone zikisalia kusombwa na maji

Mshauri huyo wa Gavana aliwataka wakaazi kumchagua kiongozi atakaueendeleza maono ya Gavana Oparanya baada ya kipindi chake kutamatika

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE