Kufwatia utata unaozidi kushuhudiwa  kuhusu chanjo dhidi ya virusi vya CORONA kanisa la Redeemed Christian Center Kanda ya Magharibi sasa linaitaka serikali kutathmin upya chanjo hiyo kabla ya kuendeleza zoezi hilo

Askofu wa kanisa hilo Andrew Wafukho amesema kuwa yafaa zoezi hilo kusitishwa na ili chanjo hiyo idhibitishwe kuwa ni salama kwa afya kabla ya kuendeleza kutolewa kwa Wakenya 

Kuhusu swala la BBI  Wafuko amejiunga na wanaoshinikiza maafisa wa utawala wakiwemo machifu ma DO na makimisha wa kaunti kujiondoa kwenye zoezi hilo na badala yake kuwaachia Wakenya kupigia debe mswada huo

Askofu huyo amechukua Fursa hii kuwatakia wataihiniwa kote nchini kila laheri wanapoanza mtiani wao Wiki lijalo

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE