Naibu chifu wa kata ndogo ya Kakunga eneo la Malava kaunti ya Kakamega Jackson Wambulwa amewataka wakazi kuzingatia marufuku ya denzi za usiku kwenye hafla za matanga maarufu kama Disco Matanga

Akihutubu kwenye mazishi ya Samwel Chikwanyi kijiji cha Shianda, Wambulwa amesema Disco Matanga imeathiri jamii pakubwa hasa nidhamu ya vijana na ametangaza kuwachukulia hatua wamiliki wa mitambo iwapo watapatikana

Aidha Wambulwa amewataka wakazi ambao walisajili kadi za Huduma Namba katika wadi kata hiyo na wamehamia sehemu zingine kujitokeza na kuzichukua kwani imekuwa vigumu kuwapata

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE