Huku serikali ikiwekea vikwazo vipya  vya kupunguza  mkurupuko wa corona nchini kwa takribani kaunti  13 kote  nchini, sasa imeshauriwa kufikiria upya katika swala hilo

Kulingana na mwanasaikologia  Phillis Kibiriti katika kaunti ya  Busia  masharti hayo mapya hayalemazi tu ukanda huu wa magharibi kiuchumi bali ina madhara makubwa kwa saikologia haswaa ya  wanainchi waliolemewa na mzigo wa kiuchumi

Kiberiti amehoji kuwa hayapingi masharti hayo mapya moja kwa moja ila anapendekeza kuwa masaa ya kuanza curfew ingesongeshwa mbele kidogo ili kumpa mwanainchi wa kawaida  nafasi ya kurejea nyumbani bila kuhangaishwa huku akisema kuwa masaa yaliyowekwa ya saa moja jioni ni mapema mno

Kuhusiana na swala la kuyafunga maeneo ya kuabudu,Kibiriti ametilia shaka uamuzi huo huku akimrai rais Uhuru Kenyatta kukaa chini na viongozi wa kidini na kuutathmini upya msimamo huo

Ikumbukwe kuwa viongozi wa kidini wameukashfu uamuzi wa Rais Kenyatta kuyafunga maeneo ya kuabudu huku wakiutaja kama usio faa.

By Hillary Karungani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE