Muungano wa makanisa NCCK kanda ya Magharibi unaitaka serikali kutafuta mbinu bora za kukabili maambukizo ya corona pasipo kuyakwamisha maisha ya wakenya

Wakiwahutubia wanahabari baada ya mkutano wao mjini Kakamega kupitia kwa naibu mwenyekiti askofu Sinema Bamba wamesema kufunga nchi bila kuwapa wananchi suluhisho la hali ngumu ya maisha hakutazuia msambao huo

Viongozi hawa wa kidini vile vile wanazitaka idara husika za serikali kuthibiti makali ya kisiasa na kuwachukulia hatua wale wanaochochea uhasama ambao unaweza kuitumbukiza nchi hii kwa machafuko

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE