Kulingana na baraza la magavana,serikali, za kaunti zitalazimika kufungwa.ifikiapo tarehe ishirini na nne mwezi wa sita mwaka wa elfu mbili ishirini na moja kabla  wizara ya uwekezaji kulipa shilingi bilioni mia moja na mbili nukta sita wanazomiliki.

Huku akihutubia umma,naibu wa kamati la magavana  bwana Martin Wambora siku ya Jumatatu aliilaumu wizara ya uwekezaji  kwa kutowajibika ipasavyo kikatiba.

Wambora ambaye pia ni gavana wa Embu alisema kuwa wizara ya uwekezaji bado haijawalipa pesa hizo ilihali zimesalia wiki mbili tu kufika mwishoni mwa mwaka wa kifedha.

Gavana Wambora  alisema pia hali hii imechangiwa na matakwa  ya serikali za kaunti malipo yaliyopangwa  kwa ajili ya  mwaka wa kifedha wa kati   wa elfu mbili ishirini  na ule wa ishirini na moja ulioafikiwa na wizara ya uwekezaji  na  kuidhinishwa na seneti  kulingana na kauli ya usimamizi wa umma wa fedha  .

Wambua alisema kuwa pesa hizo bilioni mia moja na mbili nukta sita zimegawika ifwatavyo;bilioni tatu nukta tano zafaa kulipa kaunti ya Nairobi kama salio la mwaka wa kifedha waelfu mbili kumi na tisa  hadi ule waelfu mbili ishirini na ishirini .shilingi bilioni mbili nukta tatu zafaa pia kulipa kaunti ya Nairobi ambazo zilifaa kutumika januari na bilioni moja nukta nne ambazo ni za februari

Shilingi bilioni kumi  na nne nukta nne yafaa kulipa  kaunti ishirini na tano kwa minajili ya mwezi wa tatu huku ishirini na nane nukta tano ikilipwa kwa kaunti kumi na saba kwa ajili ya Aprili,bilioni ishirini  na tano nukta tatu kwa mwezi wa tano na mwisho bilioni ishirini na sita nukta tisa kwa mwezi wa sita..

By Mary Owano

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE