Mchungaji wa shule ya msingi ya Amalemba PAG Victor Amudavi amepongeza ushindi wa kituo hiki cha 102.2mhz Lubao FM kwa kutawazwa radio bora nchini kwa vipindi vya watoto
Akizungumza na kituo hiki katika mji wa Kakamega mapema hii leo,Amudavi ametoa changamoto kwa wizara ya elimu katika kaunti ya Kakamega kuweka uhusiano mwema na kituo hiki ili kuendeleza kuguza vipaji vya watoto mbalimbali
Amudavi amepongeza wakuu wa kituo hiki pamoja na wanahabari kwa ueledi wa kazi nzuri ambao ulipelekea kwa kupata ushindi huo
Hata hivyo amudavi ametoa changamoto kwa sehemu za kuabudu kushirikiana na kituo hiki pia kulea vipaji vya watoto kanisani
By Javan Sajida