Maafisa wa afisi ya bima ya afya NHIF tawi la Bungoma pamoja na wateja wao zaidi ya 40 wamepokea chanjo dhidi ya virusi vya corona
kulingana na Collins Nyaranga mhudumu wa afya kutoka hospitali ya kibinafsi ya Foundation Healthcare ambaye alikuwa akipeana chanjo hiyo ,idadi ya waliojitokeza kuipokea chanjo hiyo ni ya kuridhisha
hivyo basi amewataka wakenya kukubali kupokea chanjo hiyo haswaa wale walio na magonjwa ambatanishi kama vile kisukari na saratani ili wajizuie na maambukizi mbali na kuisaidia serikali kudhibiti maambukizi hayo
waliopokea chanjo hiyo wameelezea sababu za kukubali kupokea chanjo hiyo licha ya hofu inayosambazwa kuhusiana na chanjo hiyo
Hata hivyo wamelezea kuwa na maswali mengi wanayohitaji kung’amuliwa
By Hilary Karungani