Familia moja katika kijiji cha Wetai inamrai gavana Wycliffe Oparanya kuingilia kati na kufuta deni la shilingi elfu mia mbili baada ya mama kupoteza maisha kwa uzazi katika hospital kuu ya Kakamega
Alex Abwenje anasema mkewe amefariki na kuacha mtoto ambaye anahitaji kushughulikiwa na hali duni ya mapato haimwezeshi kugharamia pesa hizo
Ni usemi uliotiwa mhuri na wakazi wa eneo hilo wakisema kijana huyo anapitia hali ngumu huku akihitajika kumlea mtoto
By Linda Adhiambo
