Migomo ya mara kwa mara miongoni mwa wafanyikazi wa sekta mbali mbali humu nchini ndio sababisho la migomo  inayoshuhudiwa miongoni mwa wanafunzi,

Ni usemi wa padre wa parokia ya kanduyi kaunti ya Bungoma Dominic Osianji

Akizungumza kwenye  hafla ya mazishi ya mwendazake nduguye mbunge wa Kanduyi Kizito Wafula huko Ranje kwenye eneo   wakilishi wadi ya Bukembe mashariki eneo bunge la Kanduyi, Padri Osianji amesikitikia matukio ya hivi punde ya ukosefu  wa nidhamu  miongoni mwa wanafunzi huku akikariri kuwa wizara ya elimu inahitaji kuweka  mbinu mbadala ya kukabiliana na visa hivyo bila  kuekea wazazi gharama ghali inayotokana na visa hivyo

Wakati uo huo padre  huyo ametoa changamoto kwa wazazi kuwa  waangalifu  kwa wanao haswa likizo nyingine ya wanafunzi inapokaribia huku akitaja visa vya uaviaji mimba miongoni mwa wanafunzi wa kike  kama   moja wapo ya mbinu zinazotumika  na jamii kwa ujumla  ili kuendeleza uovu.

Usemi wa padre  Osianji unakuja siku chache baada ya kuibuka mjadala mkali wa kurudisha adhabu ya kiboko shuleni,usemi unao onekana kukinzana na pendekezo hilo

Ikumbukwe kuwa tangia kufunguliwa kwa shule baada ya kipindi kirefu  cha likizo isiyo ya kawaida iliyosababishwa  na mkurupuko wa virusi hatari vya covid_19 mapema mwaka jana,shule nyingi kote nchini zimeshuhudia  visa vya utovu wa nidhamu huku kaunti ya Bungoma ikiorodheshwa miongoni mwa kaunti zilizoadhirika pakubwa kutokana na visa hivyo.

Story by Hillary Karugani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE