Viongozi wa chama cha ANC katika kaunti ya Kakamega wameanzisha

Mikakati ya kusajili wanachama wapya wakilenga kukipa chama hicho

Nguvu mbele ya uchaguzi mkuu mwaka ujao.

Wakiongea mjini Kakamega wakiongozwa na mkurugenzi wa ANC

Kaunti hii Isaac Otiende, wamesema lengo lao ni kuhakikisha kinara

Wa chama hicho Musalia Mudavadi anapata wafuasi wengi

Akijitayarisha kumenyana na viongozi wa vyama vingine kutwaa kiti

Cha urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Kauli hiyo imeungwa mkono na kiongozi wa vijana eneo bunge la

Lurambi Joel Okwako na mwakilishi wa wanawake Ruth Ombayo.

Haya yanajiri siku moja tu baada ya mwenyekiti wa ANC kaunti hii Titus

Khamala kudokeza kuwa zoezi hilo la usajili litazinduliwa rasmi

Mwezi Agosti mwaka huu.

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE