Mkaguzi wa serikali kuu Nancy Gachungu azuru kaunti ya Kakamega kuikagua mirandi iliyoanzishwa na serikali hivyo chini ya gavana Oparanya.

Akiwahutubia waandishi wa habari  nje  ya makao makuu  ya  afisi za kaunti hiyo baada ya kukutana na mawaziri wa kaunti hiyo pamoja na jopo maalum la wakilishi wadi,Nancy amesema lengo lao kama afisi ni kuhakisha  miradi iyoanzishwa na serikali hiyo imekamilika kwa wakati.

 Aidha mkaguzi huyo wa serikali kuu ameipongeza serikali ya   kaunti ya  Kakamega  kwa kutoa  mahali pa kujenga afisi zao jambo litakalorahisisha utenda kazi wao katika uliokuwa mkoa wa  magharibi kwa  ujumla.

 Miongoni mwa miradi waliyoikagua ni pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Kakamega, uwanja wa michezo wa Bukhungu miongoni mwa mingine.

Kwa upande wake naibu gavana prof Philip Kutima ambaye amekuwa mwenyeji wa maafisa hao amedokezo kuwa lengo la mkaguzi lilikuwa tu kuangazia miradi inayotekelezwa na serikali ya kaunti ya Kakamega bali si kitu kingine tofauti.

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE