Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero mwenye umri wa miaka 32, anataka kupandisha cheti ya ufungaji Ligi ya Primia, hatua ambayo inaweza kusaidia Chelsea katika azma yao ya kumsajili Muajentina huyo wakati mkataba wake unamalizika msimu wa joto. 

Aguero yuko tayari kukosa ligi ya mabingwa msimu ujao ili asalie ligi ya primia huku Chelsea na Tottenham zikiwa miongoni mwa vilabu atakavyovifikiria.

Hayo yakijiri Manchester United inaweza kujiunga na Liverpool katika mbio za kupata sahihi ya mlinzi wa kati wa RB Leipzig Ibrahima Konate. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 anatarajiwa kugharimu kiasi cha takribani pauni milioni 34. 

Manchester city walijikatia tikiti baada ya kushinda hapo jana mabao mawili kwa moja dithi ya Dortmund huku Liverpool wakichabangwa magoli matatu kwa moja na Real Madrid huku Leo ikiwa na zamu ya Chelsea kuwika katika ligi hiyo ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE 

By Samson Nyongesa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE