Viongozi wa ANC eneo bunge la Lurambi wanaitaka serikali kuona kwamba mikopo inayochukuliwa kwa ajili ya janga la corona inawafaidi wakenya mashinani

Wakiongea katika wadi ya Butsotso Mashariki kupitia kwa mwenyekiti Musa Rajab wamesikitikia kiwango kikubwa cha ubadhirifu serikali huku wakenya wakisumbukana kiuchumi.

Rajab amewataka wakenya kumuunga mkono  kinara wa ANC Musalia Mudavadi kama kiongozi pekee mwenye tajriba ya kufufua uchumi

 Kiongozi wa akina mama katika chama cha ANC eneo la Lurambi Ruth Ombayo ameitaka wizara ya afya katika serikali ya kaunti ya Kakamega kutoa chanjo ya corona kwa usawa bila kuwabagua wananchi

Bi Ombayo vile vile amewataka wakenya kuzingatia magizo ya afya kuepusha msambao wa virusi vya corona 

Wakati uo huo bi Ombayo amewataka wagombea wa nyadhifa za uongozi kupitia chama cha ANC kudumisha amani huku akiwahakikishia haki katika zoezi la mchujo

  By Linda Kefa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE