Mama mmoja kutoka eneo la Lukoye Marama Kaskazini Butere anaitaka serikali kuchunguza kile kilichopelekea mumewe kugonjeka ghafla na kupoteza fahamu baada ya kujiburudisha na wenzake
Alice Amwayi anasema mumewe Philip Amwayi alikuwa na wenzake walipoenda kwa hafla ya matanga eneo la Khwisero na alishangazwa kupata ripoti kuwa ako kwa nyumba hali mahututi na kumkimbiza katika hospitali ya Mwihila ambako anapokea matibabu.
Bi Amwayi anasema wendani wake ni watu wanaofahamika lakini anahofia usalama wake iwapo atawaripoti kwa polisi
Story by Richard Milimu