Huku shule zikifunguliwa rasmi kwa muhula wa kwanza  wito umetolewa kwa serikali kuziangazia shule za kibinafsi wakati inagawa vitabu vya kusoma kwa wanafunzi almaarufu [text books]

Ni usemi wa mkurugenzi wa shule ya kibinafsi ya Little Friends  mjini Bungoma  Mourice Wanyonyi huku akikariri kuwa wanafunzi wote wanafaa kuhudumiwa sawa na serikali bila kujali misingi ya shule.

Mgurugenzi huyo aidha  amesema kuwa kwa muda mrefu kumekuwa na dhana kuwa wanafunzi wanaosomea shule za kibinafsi wanajiweza kifedha jambo ambalo amesema kuwa  halina msingi wowote wa ukweli.

Kulingana na maswala ya wanafunzi wa grade five kurejea shuleni baada ya likizo ndefu nyumbani  mgurugenzi huyo ametoa wito kwa walimu kuwa makini na wanafunzi hao ili kuhakikisha kuwa wamerejelea masomo sawa sawa.

Ikumbukwe kuwa swala la wanafunzi wa grade five kukaa nyumbani kwa mda mrefu  limesemekana na baadhi ya waalimu kuadhiri pakubwa  hali yao  ya kimasomo huku baadhi ya waalimu wakifichua kuwa  baadhi ya wanafunzi hao huenda hawakua wakijisomea nyumbani.

By Hillary Karungani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE